Friday, August 26, 2016



Waebrania 10:19-20
"Basi ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyohai, ipitayo katika pazia, yaani mwili wake."

Kuingia patakatifu ni kuingia chumba cha enzi ya Mungu, tukumbuke kuwa Mungu ni Mungu mwenye enzi, Mtawala wa Mbinguni na Duniani.  Mtu anayeingia mahali patakatifu anapaswa awe na ujasiri wa kusimama mbele ya Mungu.  Ujasiri huo tunaupata katika damu ya Yesu Kristo ambayo ndiyo inayotutakasa na uovu wetu wote

1 Yoh 1:7
"Bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, yatusafisha dhambi yote,"

Tunajua ni muhimu kuwa safi kabla ya kuingia mahali patakatifu pa Mungu kama Taifa la Israeli lilivyokuwa likifanya hekaluni.  Na sasa katika Yesu Kristo ambaye bdiye kuhani wetu mkuu, yeye anatuongoza katika kuingia mahali patakatifu pasipotengenezwa na binadamu ila Mungu mwenyewe tukiwa safi na ujasiri wake.

Ipo njia ya mtu kupita na kuishi ili aweze kuingia mahali patakatifu, njia mpya na ni hai, hiyo njia ndiyo ipitayo katika pazia la mahali patakatifu na njia hiyo ni mwili wake Yesu Kristo.  Tukumbuke Kristo alisema kuwa yeye ni njia, na ukweli, na uzima, na hakuna afikaye kwa BABA (MUNGU) ila kupitia kwake tu.

Yohana 14:6
"Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi."

Hivyo ni vema kumjua Yesu Kristo ili tuweze kumjua Mungu, pia tumfikie Kristo na kuishi ndani ya Kristo ili tuweze kumfikia Mungu na kuishi ndani ya Mungu.  Katika Mwili wa Yesu Kristo, kanisa, ushirika na Roho wa Mungu, tunaimarika ili tuweze kupita katika pazia la mahali patakatifu na kuweza kusimama mbele yake Mungu kama Baba yetu na siyo Mhukumu wetu wetu.

Upendo wa Mungu kwetu ni MKUBWA SANA, na ndani ya Yesu Kristo Pendo la Mungu limekamilika daima na milele.  Mungu hapendi watu wake wawe mbali naye, aidha watu hao ni wakristo au bado hawajaamini ndani ya Neno la Mungu, Habari njema kwa ulimwengu wote.

Mungu ametupatia Mwana wake wa pekee Yesu Kristo ili tuokolewe kwake, tudumu katika pendo lake na kuishi katika umoja naye.

Ewe binadamu, chukua muda hu kusali sala hii fupi hata kimoyomoyo kama upo katika mazingira au ugumu wa kutoweza kuisema kwa sauti ya kinywa chako, kwa maana Mungu anasikia hata yale ya Moyoni mwa Mtu.  Na Mungu ambaye ni mwaminifu atakusamehe ya kuyafungua maisha yako katika safari mpya ya kuishi pamoja na Kristo, na katika mwili wa Kristo.

Hata kama wewe ni Mchawi au Jambazi au umetenda uovu mwingi mpaka una mashaka ya kuongea mbele za Mungu, Kristo Yesu alikuja duniani na mpaka leo yupo na Mungu ili uwe huru, Yesu Kristo wagonjwa wanaoelemewa na dhambi  na uovu wa Dunia hii na Shetani mwovu wapate kupona kwa kupokea tiba ya wokovu wake na kufanyika viumbe wapya, wawe na ufufuo wa Mungu na uzima wa milele wawe nao tele.


SALI SALA HII

Mwenyezi Mungu naomba unisikie,
na kwa huruma zako nyingi nifadhili Roho yangu.
Naungama kwako uovu wangu, nakuomba unioshe
kwa Damu ya Yesu Kristo,
yeye ambaye ni Kweli, ni njia, na Uzima.
Yesu naomba unipokee niishi upya ndani yako,
na katika ufalme wako Mbinguni.
Nidumishe nawe ili niweze kuingia mahali pako 
PATAKATIFU.
Niponye mauti ya dhambi zangu, niwekee uzima wako
wa milele ndani yangu.
Nakuomba kwa Jina lako Takatifu
YESU KRISTO.

AMINA.


Shirikisha fundisho hili na sala hii pia kwa wengine,
na Mungu akubariki na kukutegemeza daima katika Yesu Kristo.

Friday, August 12, 2016




MFANO WA MPANZI:

Katika Injili ya Mathayo sura ya 13:4-9
"Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilzianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila; nyingine zikaanguka penye miamba, pasipokuwa na udongo mwingi; mara zikaota, kwa udongo kukosa kina; na jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka.  Nyingine zikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea, ikazisonga; nyingine zikaanguka penye udongo muri, zikazaa, moja mia, moja sitini, moja thelathini.  Mwenye masikio na asikie."

Yesu  anafundisha kuhusu mfano wa mpanzi wa mbegu ambao ni mfano wa neno la Mungu kama mbegu yake katika maisha ya watu.  Katika kuelewa mfano huu, tunapata mwanga wa kuweza kujua ustawi na Neno la Mungu katika mioyo yetu na pia kujua vitu vinavyoweza kuzuia ustawi wake.  Hivyo pi tunaweza kupata mwanga wa jinsi ya kuomba juu ya Neno la Mungu kwa ajili yetu tupate msaada wake.


MBEGU ZA NJIANI:
Yesu Kristo anatafsiri kuhusu mfano kuwa mbegu zilizoanguka njiani na ndege wakazila nia watu ambao wanalipokeao Neno la ufalme wa Mungu wasilielewe naye yule mwovu akalinyakua lililopandwa moyoni mwake.

Kuna umuhimu mkubwa wa watu kupata uelewa wa Neno la Mungu, kuanzia yule alisemaye kwa watu, na pia wale wanaolisikia Neno hilo na kulipoke ili mwovu asiweze kuliiba neno hilo toka kwao. Kwa sababu neno hilo la Mungu laweza kuwa neno la tumaini au neno la uponyaji au liwe neno la kutubu; hivyo kama shetani akiweza kuliondoa kwa sababu mtu huyo aliksa uelewa wa neno hilo, basi halitozaa matunda kwa sababu halitokuwa nae tena.  Hivyo ni jambo la msingi sana wa tu wa Mungu kuomba juu ya yafuatayo:
  • Nguvu ya Mungu katika uelewa wa Neno lake takatifu, pia katika uelewa huo, watu wa Mungu waombe juu ya Uhuru wa fikra na fahamu za watu ili wasiwe wagumu katika kuelewa neno la Mwenyezi Mungu.
  •  Kusimama kinyume katika dhidi ya mashambulizi ya Adui kwa watu wa Mungu katika kuliiba neo la Mungu kwako na kuwafanya wawe wapotofu na viziwi na Neno la Mungu kwa sababu hawaoni likizaa katika maisha yao.
  • Kumwomba Mungu katika kuwafanyia watu hawa mioyo mipya ya maisha yao ili wasiwe watu wa njiani ambao hupitwa nakushambuliwa na adui wa wokovu wa Mungu.
  • Kuomba Mungu awazungushie ulinzi wake watu hawa na mioyo yao ili wawe na usalama wa neno apandalo ndani yao liweze kuzaa matunda.
Hivyo watu wenye mioyo ya njiani wazidi sana kumtafuta Mungu katika kuzidi kumjua na kumwamini Yesu Kristo nao wokovu wao utakamilika daima na milele katika jina la Yesu kristo.


MBEGU ZA MIAMBA:
Katika ufafanuzi wa mfano wa mpanzi kuhusu mbegu zilizopandwa katika ni wale watu ambao hulipokea neno la Mungu kwa furaha, lakini kwa sababu neno linakosa mizizi ndani yake, linadumu kwa muda tu.  Ila ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile mtu huyo huchukizwa na kugeuka moyo kuliacha neno hilo.

Watu hupitia ugumu wa namna hii katika kustawi kwa Neno la Mungu maishani mwao kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.  Watu wa namna hii wanahitaji maombi ya ukombozi sana kwao , lakini pia wanahitaji malezi ya karibu ili waendelee kuelewa zaidi kuhusu Mungu na Kristo wake akiyetupa ulimwengu tuokolewe.  Watu ambao wana ugumu kama miamba katika kuzaa matunda ya neno la Mungu wana tabia zifuatazo.
  • Majivuno.  Watu hawa ni wagumu kujishusha mbele za Mungu, wala kunyenyekea kwao ni kugumu pia.  Ni katika kunyenyekea mbele za Bwana Yesu Kristo ndipo kutakapowaweka huru nafsi zao, na hapo wataweza kuanza kuzaa matunda pia.
  • Shingo Ngumu.  Hapa ni kuhusu watu kushindwa kuacha mambo ya kale, kushindwa kuacha dhambi na pia kujiona kuwa wapo sawa katika kila jambo, hata kama wakikoseana na watu wengine, wao huwa wagumu kusamehe au kuomba msamaha.  Shingo ni ishara ya kukataa Utiisho wa Nguvu Ya Mungu katika maisha yako.
Kwa kufuata mwenendo wa Roho Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu (Wagalatia 5:16-26), ndipo wataweza kuishi katika uhuru na kuweza kuyafanya mazuri yaletayo matunda ya Neno la Mungu liishilo ndani yao.


MBEGU ZA MIIBA:
 Katika mfano wa mpanzi, Yesu Kristo anaelezea kuhusu mbegu zilizoanguka katika miiba kama vile mtu aliyepandwa katika miiba ila kutokana na shughuli za Dunia na udanganyifu wa mali, Neno la Mungu ndani yake halizai kutokana na msongamano wa vitu hivyo maishani mwake.

Watu wanaosongwa na miiba wanashindwa kuachia shughulli za maisha yao ya kila siku ili wajitoe katika kutumika katika Yesu Kristo.  Hivyo wanshindwa kuzaa matunda kwa sababu wanaona kumtumikia Mungu kwa kuacha vitu vyote maishani mwao ni Upotofu, au wanaona kuwa wanaweza kumtumikia pamoja na mali zao pia.  Watu hawa wanaweza kuwa sifa zifuatazo:
  • Elimu kubwa na Nafasi kubwa katika maisha yao na jamii inayowazunguka pia.  Hivyo waogopa kupoteza utajiri na heshima ambayo wamejijengea katika maisha yao.
  • Wanasifiwa na watu wengi kwa yale ambayo wameyafanya maishani na katika jamii.  Wanapata utukufu toka kwa watu wengine katika mambo waliyoyafanya duniani, hivyo kuyatelekeza hayo kwa ajili ya Yesu Kristo inakuwa vigumu sana kwao.
  • Wasemaji Wakuu katika Jamii.  Watu hawa wanaweza kuwa na nafasi kubwa za kuwafanya watu wawasikilize katika yale wanayosema.  Wanashiriki vikao vikubwa na wakuu na wana wafuasi wengi wanaowapenda wao na kupenda kazi zao pia.  Wamejivunia utajiri katika hayo yote na hivyo kuyaacha inakuwa vigumu sana kwao.
Watu hawa wanahitaji msaad awa Mungu ili waweze kuwa huru na mambo yanayowazunguka, ni katika upendo mwingi na neema kuu ya Mwenyezi Mungu ndipo watu hawa watapokea Uhuru wao katika Kristo, hivyo ni muhimu sana kuomba Mungu akutane nao katika maisha yao ya kila siku na kuleta mabadiliko.  Ni vema kuomba Mungu aishinde hofu ifunikayo mioyo na fikra zao, kwa sababu wengine wanaogopa kukana shughuli hizo wakiogopa mikataba yao ya Gizani na yule shetani, mwovu au wakiogopa kifo walichoahidiwa kama wakimkana shetani na kumfuata Yesu Kristo.


MBEGU ZA UDONGO MZURI:
Katika mfano wa mpanzi, Yesu Kristo anafafanua kuhusu mbegu zlizoanguka katika udongo mzuri, kama vile watu walisikiao Neno la Mungu, wakalielewa na kulishika, hivyo wao huzaa matunda kwa viasi vyao.   Katika kundi hili, watu wa Mungu ni wa le wawekao bidii katika Neno la Mwenyezi Mungu ndani yao ili liweze kuzaa matunda katika maisha yao ya kila siku.

Watu hawa wanapata uelewa wa Neno la Mungu na linadumu mioyoni mwao.  Watu haw ni wanyenyekevu na pia ni watulivu mbele za Bwana.  Wanao ulinzi wa Mungu dhidi ya Jua na Miiba ya ulimwengu huu, kwa sababu kama vile walivyo katika udongo mzuri, Mwenyezi Mungu amewatenga watu hawa na miyo yao mabali na mambo yanayozuia Ustawi wa Neno lake ndani yao, na mioyo yao pia siyo miamba migumu tena, ndiyo maana ni waelewa wa neno la Mungu na wanaweza kuliishi na kulifuata daima.

Watu hawa wanafuata mwongozo wa Roho Mtakatifu katika mienendo ya maisha yao.  Pia ni washindi dhidi ya mashambulio ya Adui mwovu katika kuwanyang'anya Neno lililo ndani yao kwa maana Mungu yupo pamoja nao wote watembeao katika Njia ya Yesu Kristo daima.

Mtu akiishi katika mfano wa mbegu za Udongo mzuri, ni kwamba anishi maisha yayompendeza Mungu, na ni dhairi kuwa yupo Imara katika maombi mbele ya Mungu na anadumu katika kukua na kustawi mbele ya Mungu kwa mbegu za Neno la Mungu ndani yake. 
Watu hawa wanatabia zifuatazo:
  • Wanadumu katika kutafakari Neno la Mungu maisha yao yote mchana na Usiku.(Zaburi 1)
  • Wanadumu katika maombi bila kukoma ila kuweza kupata Msaada wa Mungu kila siku.(Efeso 4).
  • Wapo Imara dhidi ya vita vya Ufalme wa Giza wakivaa silaha zote za Mungu (Efeso 4).
  • Wanaenenda katika Roho Mtaaktifu na siyo katika mambo ya kidunia(Wagalatia 5).
Watu waaminifu wa Mwenyezi wanayo matumaini juu ya kile walichoahidiwa na Mungu katika Neno la Mungu, ikiwa ni Uzima wa milele na Ufalme wa Mbinguni na pia Mateso ambayo yote ni katika njia ya Uzima na Ukweli na  kumtukuza Mwenyezi Mungu.


NAOMBA USHIRIKI SALA HII:

"Mungu Mwenyezi nashukuru kwa muda ambao umenipa duniani, naomba kwako unijalie uelewa wa Neno na Kweli yako. Naomba unijali kustawi katika kukujua na kukuamini wewe ili nidumu nawe.  Nifunulie zaidi kuhusu mwanao Yesu Kristo na Nuru yako iongoze maisha yangu daima katika Jina la YESU KRISTO...AMINA."


NASHUKURU SANA KWA KUCHUKUA MUDA KUSHIRIKI NENO HILI.  MUNGU AKUJALIE UELEWA MWINGI NA AKUBARIKI DAIMA KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NA NURU YAKE IANGAZE JUU YAKE DAIMA...AMINA.

Tuesday, May 10, 2016



Umewahi kujiuliza ni kwanini kuna watu wakienda mbele za Mungu wanapokea na wengine, hawapokea ?,Yumkini mara nyingi sana unatamani Mungu akutane na wewe mara tu uendapo hemani mwake, kweli kabisa mahili alipo weka kumbukumbu la jina lake ndipo mahali ambapo Mungu huwabarikia watu wake na kuwaponya magonjwa yao.

Kutoka 20:24
"Kila mahali nitakapotia ukumbusho wa jina langu, hapo ndipo nitakapo kujilia na kukubarikia."


Kumbe ni haki yako Mungu anapobadilisha maisha yako mahali ambapo amepachagua aliketishe jina lake, haiwezekani ukawa ni muhudhuriaji mzuri wa mahali ambapo jina la Mungu limekaa na maisha yako yakawa vilevile, ukiona hivyo ujue kosa si la Mungu, kuna vitu wewe mwenyewe hujaviweka sawa mbele za Mungu, Mungu anataka kila uhudhuriapo mbele zake maisha yako yageuzwe, usiwe kama vile ulivyo lakini wewe toka umeanza kusali sasa ni miaka mingi, lakini maisha yako yapo vilevile, hatuoni Baraka ambazo, Mungu amewahaidi wampendao kwenye maisha yako, kumbuka umaskini si fungu lako, madeni si fungu lako wewe ni mtu unayeshinda mbele za Bwana.Ni kwa muda mrefu sasa ugonjwa ule ule unaumwa na kila siku unapita mbele kuombewa wala hupokei, huoni kupona kwako, na pia kuna watu wanaumwa ugonjwa unaofanana na wewe wao wanakuja tu kidogo wakiombewa wanafunguliwa na kutoa ushuhuda, kwasababu liko tatizo kwako ndo maana hupokei ujihudhurishapo mbele za Mungu.

Mungu anataka ufike mahali usiende kwenye uwepo wake kimazoea lazima ujue kwamba kuna viwango vipya naviingia kila niendapo mbele za Mungu. Musa alipo kuwa anarudi kutoka mlimani mbele za Mungu, maisha yake yalibadilishwa, akawa anang’aa, hadi watu wakaogopa kumwangalia usoni pake, huwezi uakaenda mbele za Mungu na maisha yako yakawa vilevile ipo nguvu ya mabadiliko.

MAANDALIO YA MOYO.

Watu wengi walichokosa ni maandalizi, wanakwenda mbele za Mungu pasipokujiandaa, ndiyo maana hata wakienda hawapokei miujiza yao.


Mithali 16:1
"Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu. Bali jawabu la ulimi latoka kwa Bwana."

Sikuzote katika maisha ili mambo ya mtu yaende vizuri yanategemeana na maandalizi aliyoyafanya, kama mtu anaharusi ili arusi yake iwe nzuri itategemeana na maandalizi yake, waweza kujiandaa kwa muda mrefu lakini tukio likawa la muda mfupi, harusi inayofanyika kwa siku moja inaweza ikaandaliwa mwaka mmoja, au zaidi, mtihani unaoufanya kwa siku moja unaweza ukajiandaa kwa mwezi zaidi ya mmoja. Kumbe lipo jawabu la Mungu kwa mtu anaye jiaanda vizuri anapohuria mbele za Bwana.Mungu anajibu sawasawa na maandalizi yako, ndiyo maana wengine wanapokea na wengine hawapokei.Uendapo mbele za Bwana moyo ndiyo unaopokea, Mungu akifika anaagalia moyo wa nani umejiandaa kupona, huo uliojiandaa kupona ndiyo unaopona, moyo wa nani umejiandaa kubarikiwa ndiyo unaobarikiwa, kama moyo wako haujajiandaa vhochote Mungu akufanyii chochote, maana Mungu ni Mungu aangalie moyo wa mtu na wala si umbo la nje na ndoomaana habagui kila mtu anampa kulingana na moyo wake ulivyojiandaa.

Friday, April 29, 2016


VITU NA WATU WALIOMGUSA MUNGU.
  Tunaposema mwanamke alligusa mavazi ni kwasababu kuna vitu na watu ambao Yesu anawatumia kama mavazi yake,ikiwa umefanya vitu kwao wakafurahi unaruhusu nguvu ya Mungu ipitie wao na kubadilisha maisha yako,ninaposema hayo nina maana hii si kila mtu au kila kitu kimemgusa Mungu,kwamaana hii kuna wengine unaweza ukawagusa kama vazi la Yesu na nguvu za Mungu zisikuhudumie lakini kuna vitu na watu wengine wao wamegusa ngozi ya Yesu ukiwagusa hao hutokuwa kama vile ulivyokuwa ambao ni:

                            i. Watumishi wa Mungu.

Watumishi wa Mungu ni mavazi ya Yesu ndiyo waliomgusa Yesu wao wamebeba mabadiliko ya maisha yako ninaposema kugusa nina maana hii ukionesha kuwajali,  kula pamoja nao,watu wengi wanatamani kuguswa na nguvu ya Mungu wakiwa wamesahau kwamba.
           1Wafalme 17:13-16
“Eliya akamwambia usiogope,enenda ukafanye kama ulivyosema,lakini unifanyie kwanza mkate mdogo uniletee,kisha jifanyie nafsi yako na mwanao.Kwakuwa Bwana Mungu wa Israeli asema hivi,lile pipa la unga halitapungua wala ile chupa ya mafuta haitaisha,hata siku ile Bwana atakapoleta mvua juu ya nchi,Basi akaenda akafanya kama allivyosema Eliya,na yeye mwenyewe na Eliya na nyumba yake wakala siku nyingi.Lile pipa la unga halikupunguka wala ile chupa ya mafuta haikuisha,sawasawa na neno la Bwana kwa kinywa  cha Eliya”
     Mungu alitaka kubadilisha maisha ya mwanamke mjane maana alikuwa amekata tamaa kwasababu ya njaa ya kipindi kile lakini kanuni ya kiroho inasema uviguse vilivyomgusa.Eliya mtumishi wa Mungu alikuwa amemgusa Mungu katika utumishi wake hivyo alikuwa ni vazi la Mungu mwanamke mjane alipofuta njaa kwa Eliya naye Mungu akafuta njaa kwa mwanamke mjane,unapobadilisha maisha ya watumishi wa Mungu naye Mungu anabadilisha maisha yako maana wao wamemgusa Mungu,mwingine anaweza kusema mbona ninacho kidogo mwanamke mjane hakuwa nacho kingi ila alitoa kwa imani na  Mungu akatengeneza mipenyo.
        Si mwanamke mjane tu hata mwanamke mshunemu ambaye alikuwa tasa hazai,lakini alimpokea Elisha na kumpa chakula nakumfanyia kitanda kizuri kwaajili ya kulala bali Elisha ni mtumishi wa Mungu,vazi la Mungu amemgusa Mungu katika utumishi wake,alipompokea Elisha naye akapokea mtoto(2wafalme 4:8).Kumbuka kitendo cha mwanamke kugusa upindo wa vazi la Yesu msiba wake ulipona Gusa vilivyomgusa.
   Hata Ibrahimu Baba wa imani alikuwa amehaidiwa na Mungu kupata mtoto kwa muda mrefu sana lakini asipate,siku moja aliwapokea watumishi wa Mungu walipopita karibu na hema yake na kuwanawisha miguu na kuwapa chakula walitamka kitu kwake “Mwaka kesho wakati kama huu utapokea mtoto”(Mwanzo 18:1-10) akampokea Isaka,wapo wengi waliogusa vilivyomgusa na maisha yao yakabadilishwa,Mungu nataka akuguse na nguvu yake gusa kwanza vilivyo mgusa.


                            i.Makanisa na huduma

Makanisa na huduma mbali mbali ni vitu vilivyomgusa Yesu unapogusa ni lazima maisha yako yabadilishwe,Sulemani alimjengea Mungu nyumba,kwasababu alikuwa amegundua siri hii kwamba nyumba ya Mungu imefungamanishwa na nguvu ya Mungu na alikuwa anataka ufalme wake uwe imara alimjengea Mungu nyumba,haijawahi kutokea katika Israeli mtu aliyekuwa kama Sulemani katika ufalme wake kipindi chake hakujawahi kutokea vita,alikuwa na mahali nyingi kupita  wafalme wote duniani,alikuwa na hekima isiyoelezeka kwasababu alimjengea Mungu nyumba,angalia makanisa yanayojengwa toa mchango wako uone kama nguvu ya Mungu haijakugusa siyo mpaka mchango utangazwe kanisani ndipo  ufanye uonapo tu kuna upungufu fanya haraka ili Mungu aachilie nguvu ya kukugusa,angalia ndani ya kanisa ukiona jengo limechakaa angalia washirika utawaona nao pia wamechakaa,ukikuta kanisa limejengwa vizuri  limepambwa utakuta pia washirika wanamaendeleo kwenye maisha yao.Kwanini? ni kwasababu watu wengi hawajaigundua siri hii.
     Na hata wakati mmoja wazee wa Israeli walimwendea Yesu kwa kumtaka amponye mtumwa wa akida mmoja ambaye alikuwa hawezi,ili maombi yao yajibiwe yawe na ushawishi mbele za Yesu,walionyesha kile alichokifanya kwenye lile taifa,wakasema alitujengea na Sinagogi Yesu akapata ushawishi kwenda kumponya(Luka 7:1-6) unaweza ukawa unataka uponyaji lakini hauja ushawishi ufalme wa Mungu uachilie nguvu yake,wanao jenga makanisa nakusapoti huduma mbalimbali wanakuwa wamegusa vilivyogusa ufalme wa Mungu hivyo nguvu za Mungu zinapita kwenye huduma na kugusa maisha yao,labda hauna kazi,au unafanya biashara bila faida bali unaona madeni yanakuwa mengi,ukiona kunaujenzi wa kanisa nenda ukachangie ili uone kanuni hii ya kiroho inavyofanya kazi.


                            i.Yatima,wajane na mgeni pamoja na maskini.

Watu wengi hawajajua kwamba yatima na wajane,wageni pamoja na maskini wao ni maskini wao ni mavazi ya Yesu kwamba ukimaliza shida zao naye Yesu anamaliza za kwako,kumbuka kile kitendo cha mwanamke mwenye kutokwa damu kugusa upindo wa vazi la Yesu nguvu za Mungu zikamhudumia,Je umewahi kuapata historia ya mwanamke Dorkasi ambaye aliumwa mpaka akafa,kipindi cha uhai wake alikuwa anawajali wajane,angalia mstari huu.
   Matendo 9:39.
“Petro akaondoka akafuatana nao,alipofika wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye,wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizoshona Dorkas wakati ule alipokuwa pamoja nao”
    Soma na uelewe tabia ya mavazi ya Yesu ,hawa wajane walisimama kama mavazi ya Yesu,wakatoa sauti za kilio,vile vilivyomgusa Yesu vina sauti inayogusa nguvu inayogusa kwa wakati huo Dorkasi alikuwa hajililii lakini wajane walilia(mavazi yalilia)unaweza ukapita kwenye hali ngumu kwa kiwango ya kwamba ukashindwa kujiombea mwenyewe lakini vile ulivyowahi kuvigusa vilivyomgusa Yesu vikatoa sauti kwaajili yako,kufufuka kwa Dorkas hakukuwa kwa sababu Petro anaoupako wa kufufua wafu ila ni kwasababu Dorkasi amegusa vilivyomgusa.
           Mambo ya walawi 19:9-10
“Na mtakapovuna mavuno ya nchi yenu,usivune kabisa kabisa pembe za shamba lako,wala usiyakusanye masazo ya mavuno yako.Wala usiyakusanye masazo ya mizabibu yako yaliyopukutika uyaache kwaajili ya maskini na mgeni,mimi ndimi Bwana Mungu wako”
      Anaposema utakapoyavuna mavuno ya nchi anamaana hii kila kazi ya mikono unayoifanya ziwe ni biashara,pale ofisini pako haijarishi ni kazi gani kwa kile unacho kipata mahali hapo usisahau vile vinavyomgusa Yesu yaani maskini na mgeni,anaposema maskini anamanisha muhitaji anaposema mgeni ni Yule mtu aliyefikiapo kwenu mfano mfanyakazi wa ndani huyo ni mgeni uanapofanya kwaajili yake unakuwa umevigusa vilivyo mgusa Yesu,wengi wanawanyanyasa wageni yaani wafanyakazi wandani wasijue kwamba wamemgusa Mungu,angalia kile kilichomgusa Mungu kikinung’unika kwaajili yako maisha yako yapo hatarini,usiwasahau wajane yatima na maskini na mgeni.


                            i. Wazazi(Baba na Mama)

Wazazi ni mavazi ya Yesu wamegusa ngozi ya Yesu,hivyo wamefungamanishwa na nguvu ya Mungu,kuna mahali huwezi kufika ukiwa hujafanya kitu kwao,watu wengi wamefanikiwa lakini ukiangalia wazazi wao wanaishi katika hali mbaya,shida,umaskini, hawajui ya kwamba masononeko ya wazazi wao ni mikosi kwenye maisha yao,ili nguvu ya Mungu ikuguse nilazima uviguse vilivyomgusa hii ndiyo kanuni ya kiroho.Isaka alipoona kwamba umri wake umekwenda na macho yake yamepofuka akatakakumbariki mwanawe Esau lakini Isaka Babaye alijua kanuni ya kiroho kwamba Esau asipo vigusa vilivyomgusa hawezi akapokea Baraka za wazazi,hivyo akamwagiza amtengenezee chakula kitamu namna ile anapenda.
     Mwanzo 27:3-4
“Basi naomba chukua mata yako,podo lako naupinde wako,ukaende nyikani uniwindie mawindo.ukanifanyie chakula kitamu namna ile nipendavyo,ukaniletee ili nile Roho yangu ikubariki kabla sijafa”
   Wazazi wako wanataka ufanye kitu kwao kabla hawajafa,wengine wazazi wao wanaishi kwa shida na huku uwezo wanao ila wakifa wanapamba vizuri majeneza ilikuwaonyesha kwamba wanawajali,usijali maiti iliyokufa wajali wazazi wako wakiwa hai ili nguvu ya Mungu ikuguse,Isaka alimwambia shituka Esau nguvu za Mungu haziwezi kukugusa nikiwa nimekufa hata ukinifanyia jeneza zuri kiasi gani nikiwa hai fanya chakula kitamu kama nipendavyo nikubariki.Huwezi kupiga hatua yoyote kwenye maisha yako kama hujafanya kitu kwa wazazi wako,naye mtume Paulo hawi mbali kwamba kuna watu wanakufa leo kwasababu hawaaeshimu wazazi wao.
       Waefeso 6:2-3
“Waheshimu Baba yako na Mama yako;amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,upate heri ukae siku nyingi katika dunia”
Ni ukweli Mungu amehaidi kwamba miaka yetu ni sabini au tukiwa na nguvu themanini lakini ahadi hiyo ili itimie kwako ni lazima kwanza uviguse vilivyomgusa wazazi ukiwaheshimu wamefunga manishwa na nguvu yakuwafanya watu waishi maisha marefu.Kuna ndugu mmoja alikuafa.Kipindi cha uhai wake alikuwa na kazi yake nzuri,nyumbani kwake alikuwa amejijenga sana lakini alikufa katika umri mdogo sana hata miaka 30 hakufikisha,siku ya mazishi yake ilipofika walienda kumzika mahali alipozaliwa,watu walipotazama maisha ya wazazi wake,maana wazazi wake mahali tu wanapolala,nyumba wanayoishi imejengwa kwa mianzi na kila mmoja akawa anashangaa kwamba yeye aliishi kwenye maisha ya kifahari ia wazazi wake wanaishi kwenye maisha kama haya si angewabadilisha na wazazi wake?kumbe ndiyo maana amewahikufa,unapofanikiwa usiwasahau wazazi wako iliusiondoke mapema duniani wazazi wamebeba Baraka ya maisha marefu,namna unavyowagusa kwakufanya namna wanavyopenda wao,unakuwa sawasawa na mwanamke mwenye kutokwa damu alipovigusa vilivyovyomgusa Yesu aliongeza maisha ya kuishi duniani pamoja na kwamba alikata tamaa.


Watu wengi wanajiuliuliza nguvu ya Mungu ni nini na inawezeje kutenda kazi? Ni kwamba nguvu ya Mungu ni uwezo wa Mungu ambao unaachiliwa kwa Neno la Mungu na kuleta matokeo kama lilivyoagizwa na Mungu mwenyewe,matokeo ya Neno la Mungu ndiyo nguvu ya Mungu,kwasababu neno likitumwa linaleta mabadiliko kwenye maisha ya watu,na wengine pia wanajiuliza kwamba kuna kuguswa na nguvu ya Mungu hivi huko kuguswa kuna maana gani ?

                                    MAANA YA KUGUSWA
Kugusa ni ishara ya kuonyesha ili mtu akuonyeshe kitu anagusa ili kukudhibitishia,kukupa uhakika wa kile ambacho anakwambia,hivyo Mungu anatabia hii ya kugusa watu wake ili awadhibitishie kwamba yeye ndiye Mungu mafano inasema.

Yeremia 33:3
 “niite nami nitakuitikia na kukuonyesha mambo makubwa magumu usiyoyajua” (anaposema kuonyesha ndiyo ishara ya kugusa)

Kumbe hili neno unaweza kuliweka hivi:Niite nami nitakuitikia na kukugusa katika matendo makubwa magumu usiyo yajua,matendo makubwa magumu ndiyo matokeo ya nguvu ya neno la Mungu,hayo matokeo ya nguvu ya neno la Mungu ndiyo uponyaji,hiyo ndiyo mipenyo ambayo Mungu anaachilia kwenye maisha ya watu wake,unaweza ukawa na tatizo unahitaji kuguswa tu na nguvu ya Mungu maana yenyewa ikikugusa tu mabadikliko yanatokea kwenye maisha yako tuone mifano michache kwenye maandiko ya watu walioguswa na nguvu ya Mungu.

1)    Vipofu wawili waliomfuata Yesu  alipokuwa akipita.
Mathayo 9:27-30
Yesu alipokuwa akipita kutoka huko,vipofu wawili wakafuata wakipaza sauti,wakisema urehemu mwana wa Daudi.Naye alipofika nyumbani wale vipofu walimwendea Yesu akawaambia mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia Naam Bwana,ndipo alipogusa macho yao akawaambia kwa kadili ya imani yenu mpate,macho yao yakafunguka”.
  Kipofu ni mtu asiyeona mbele yake anaona giza,hawa vipofu wawili wanafananishwa na watu wasiokuwa na maono ambao hawana uhakika na maisha yao,hawajui walikotoka kupoje wala wanako elekea kuna hali gani? Hivyo wanaishi maisha ya kupapasa,Yesu aligusa macho yao maana yake aligusa maono yao.Nguvu ya Mungu inapojidhihirisha mahali inashughulikia maono.Mwingine yupo kwenye ndoa kwa Muda mrefu hajapata mtoto ukiangalia mbele yake anaona giza kwamba hawezi kupata mtoto,Yesu akikugusa unapata maono ya kupata mtoto,kwasababu ili shetani akupate anakuharibia maono yako na ndiyo maana vijana wengi wanaangamia kwa kukosa maono,wana macho lakini hawaoni maana maono ndiyo macho yanayobadilisha maisha ya mtu.Kumbuka nguvu ya Mungu ikimgusa mtu inashughulikia maono ya mtu,chochote unachokitaka kwa Mungu ni lazima ukione kwanza ndipo ukipate,ukiona maisha mazuri yatakuja maisha mazuri,ukiona kupona utapona,Yesu aligusa macho yakafunguka,nguvu ya Mungu ikikugusa utaona kule unakoelekea.


1) Mama mkwe wa Petro amelala hawezi homa imemkamata.

Mathayo 8:14-15
“Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro,akamwona mkwe wa Petro,mamaye mkewa maelala kitandani hawezi homa.Akamgusa mkono homa ikamwacha,naye akaondoka akawatumiakia”
Umejiuliza kwanini ?Yesu aligusa mkono homa na ikamwacha,kwanini? nguvu ya Mungu iligusa mkono wa Mama mkwe wa Petro homa ikamwacha,kumbe kuna kitu Yesu alikuwa anakishughulikia kwenye mikono ya mama mkwe wa Petro,mikono inahusika na utendaji wa kazi(kila kazi ianafanywa na mikono).Angalia sana kuna watu wengine mikono yao imebeba laana kila wanachokifanya hawafanikiwi mpaka wanapata homa,magonjwa kutokana na mkandamizo wa mawazo wakutokufikia malengo yao kama mama mkwe wa Petro,kumbuka kwamba biashara zako ni kazi ya mikono,masomo yako ni kazi za mikono,kilimo chako ni kazi za mikono na maandiko yanasema Mungu atabariki kazi za mikono,Yesu alipokuwa anagusa mikono ya mama mkwe wa Petro alikuwa anashughulikia laana iliyokuwepo kwenye mikono ya mama mkwe wa Petro.Mwambie Yesu kama alivyogusa mikono ya Mama mkwe wa Petro mwili wake ukawa salama vivyo hivyo akuguse na wewe kazi zako zikawe salama.


MAMBO MUHIMU YA KUFANYA ILI UGUSWE NA NGUVU YA MUNGU

1)Viguse vilivyo mgusa Yesu.
Marko 5:25-34
“Na mwanamke mmoja mwenyekutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili,na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi,amegharimia vitu vyote alivyonavyo, kusimfae hata kidogo bali hali yake ilizidi kuwa mbaya bali aliposikia habari za Yesu,alipitaa katika mkutano kwa nyuma akaligusa vazi lake,maana alisema nikiyagusa mavazi yake tu nitapona,mara chemchemi ya damu yake ikakauka,mara akafahamu nafsini mwake kwamba amepona msiba ule,na mara Yesu hali akifahamu nafsini mwake ya kwamba nguvu zimemtoka,akageuka kati ya mkutano,akasema ni nani aliyenigusa?  wanafunzi wake wakamwambia Je wawaona mkutano wanavyo kusongasonga,nawe wasema ni nani aliye nigusa.akatazama pande zote ili amwone yeye aliyetenda neno hilo.Yule mwanamke akaingiwa na hofu na kutetemeka,akijua lililompata,akaja akamwangukia,akamweleza kweli yote,Akamwambia binti imani yako imekuponya,enenda zako kwa amani uwe mzima,usiwe na msiba wako tena."
    Kuna nguvu katika kuvigusa vilivyomgusa,ili nguvu ya Mungu ikuguse kanuni mojawapo ya kiroho ni kugusa vilivyomgusa,mwanamke mwenye kutokwa damu aligundua hii kanuni ya kiroho akagusa upindo wa mavazi yake Yesu,nguvu zikamtoka Yesu kupitia kwenye mavazi zikamgusa mwanamke.Huyu mwanamke alitengwa na jamii yake kwasababu ya kutokwa damu na alilipa gharama ya damu kumwagika,kwa kuzunguka mahospitalini na kukutana na waganga wa kila namna lakini ugonjwa wake haukupona,ila alipopata habari za Yesu alisema nikiyagusa mavazi yake tu nitapona,angalia vizuri mavazi yalikuwa yamemgusa Yesu kile kitendo cha kugusa kilicho mgusa nguvu ya Mungu ikamfungua mwanamke,kumbuka mwanamke hakugusa ngozi bali vazi la Yesu.Vazi la Yesu limepewa nafasi ya kugusa ngozi ya Yesu ndilo limebeba nguvu inayobadilisha,na unapogusa vazi la Yesu automatically nguvu zinamtoka Yesu na kukugusa,unaweza ukawa unasema mbona naingia kanisani ila ugonjwa wangu hauponi swali ni kwamba umevigusa vilivyomgusa? Na ndiyo maana wengine wakiomba kidogo Mungu anasikia maombi yao na kuyajibu kwasababu wamevigusa vilivyomgusa hata ndani ya kanisa tutaendelea kutofautiana katika wengine watafanikiwa sana na wengine watafanikiwa kidogo kwasababu ya kutofautiana katika kuvigusa vilivyo mgusa,wataingia wagonjwa watatoka wagonjwa na wengine wazima.Hata siku ile mwanamke hakuwa mgonjwa peke yake,walikuwepo wengi lakini aliyegusa vilivyomgusa ndiye aliyefunguliwa.


         Luka 6:16
“Na makutano wote walikuwa wakitaka kumgusa,kwasababu uweza ulikuwa ukimtoka ukiwaponya wote."

Je unataka uweza wa Mungu ukifikie? mguse ili ukufikie hawa walikuwa wakimgusa na uweza wa Mungu ulikuwa ukimtoka na kuponya magonjwa yao.Watu wengi wanapenda kuombewa lakini hawapendi kulipa gharama ya kugusa vilivyomgusa,hata kama mtumishi wa Mungu anakuombea hakikisha una vigusa kwanza vilivyomgusa Mungu ili maombi yalete matokeo,haijarishi ni tatizo gani wewe gusa tu vilivyomgusa ipo nguvu inayobadilisha katika vile vilivyomgusa Yesu.Mtu anaweza akawa anajiuliza hivyo vitu vilivyomgusa Yesu ni vitu gani? Au hayo mavazi aliyoyagusa mwanamke yalikuwa yanamaanisha nini?,tuangalie kwa undani maana Roho mtakatifu anataka akufundishe kitu.

Categories

Powered by Blogger.

Popular Posts